Mimi ni mama mwenye watoto watatu na nina umri wa miaka 38. Mwaka 2018 nilimpoteza mwanaume wangu mzuri aliyekua mpambanaji sana na muwajibikaji haswa, na mpaka anafariki, alituachia nyumba mbili, moja tunakaa na nyingine tumeipangisha. Alituachia pia gari aina ya harrier pamoja na kiasi cha fedha kama 64M.
Huyo mwanaume wangu aliyefariki kazi zake alikua anafanyia migodini huko chunya, na wakati wa kumaliza msiba wake yaani matanga, mama mkwe na ndugu wengine wa mume waliamua kutochukua mali yoyote ile, walisema vyote vibaki kusaidia familia na watoto, nilifurahia uwamuzi wazo japo hiyo familia sio njaa njaa ni wanajiweza sana.
Baada ya kumaliza msiba, nilifungua duka langu la vitenge na pesa nyingine nilimgawia kaka angu na mama yangu wafanye biashara nao kujikimu maisha, kule bank pesa ziliisha kabisa lakini duka likawa linaendelea hivyo hivyo kwa kusua sua maana biashara nazo kuziendesha ni changamoto.
Kipindi hicho hicho napambana na biashara yangu ya duka, nikakutana na rafiki yangu, yeye anamishe sana sana za dubai japo sikujua hua anafanya shughuli gani haswa lakini alikua na maisha vizuri tu. Nilimsimulia yaliyonikuta ya kuondokewa na mume na mapambano yanayoendelea kwa kusua sua, alionekana kuhudhuzunishwa na changamoto hizo, akaniambia yupo tayari kunisupport kama nitaridhia.
Nikamwambia ninachotaka ni maisha mazuri kwa hiyo nipo tayari anisaidie. Akasema nitafute 70M kisha nimtafute na kama nikimpatia, ndani ya mwezi tu inakua imeongezeka mara mbili. Basi nikaliwaza hilo swala, na akili zangu za tamaa nikauza ile nyumba niliyopangisha pamoja na lile gari, nikamtumia ile pesa yote, yaani kuanzia hapo sikuwahi kumsikia tena yule dada wala kumuona mpaka leo.
Na hapo ndipo majanga yalipoongezeka zaidi, biashara yangu ya vitenge ikafa, kaka yangu nae biashara zake zikamshinda yani sikua na sehemu ya kupata msaada wa kusogeza maisha, nyumba niliuza ya kupangisha na gari juu duuuh. Ikabidi nianze kupika chakula yaani mama ntilie, na ndo kazi ninayoifanya mpaka wa leo. Watoto ilibidi niwahamishe shule waliyokua wanasoma maana ada ilikua kubwa, maana nilijaribu kuwaomba ukweni msaada wa kujiinua tena kimaisha, walikataa kabisa, lakini waliniambia kua niwape watoto wawasomeshe wao, jambo ambalo nililikataa.
Maisha yangu ni magumu sana, ingawa nakaa kwenye nyumba nzuri tu, lakini maisha ni magumu sana, najua ni ujinga wangu na tamaa ndo umenifanya niporomoke hivi, nawaasa wengine, muwe makini na marafiki feki, usikubali kuharibu vitega uchumi ulivyonavyo kisa tamaa ya mali ya kusadikika.. ni huzuni sana kwakweli. ni hayo tu.
Keep reading
Sign in to read the full confession
Create an account or log in to unlock the rest of this story.