Wazima jamani, nimekuja hapa na simulizi yangu nataka niwasimulie, jinsi ilivyonifanya nijione sina bahati ya mapenzi. nilikutana na huyu kaka, ndo yalikua mahusiano yangu ya kwanza kabisa.
Huyu kaka yeye alikua amemaliza chuo na anasubiri ajira, mimi kipindi hicho nilikua nimemaliza kidato cha nne ila sikuendelea na masomo. Basi penzi letu lilianza vizuri na kaka watu hakua na uwezo mzuri wa kifedha na alikua akiishi kwao lakini niliamini ipo siku karibuni atapata kazi na maisha yatakua mazuri.
Maisha yakaendelea, ikapita miaka miwili ya kuhangaika hangaika na mwishowe akapata kazi, tena jiji la dar maana tulikua tukiishi mkoani. mpenzi wangu akahamia dar tena aliajiriwa TRA, sasa shida ikaanza pale nilipokua namwambia kua nataka nije dar, hua ananiambia nisubiri kwanza.
Basi siku zikawa zinaenda tu, nikajisemea tu kua hapa nisipojipambania, ndoto zangu zitapotea na hakuna wa kunihurumia. Nikapambana nikaja dar, ila cha ajabu akawa ananikwepa tu muda wote, kuonana ananikwepa, na hata tukionana basi ni muda mfupi tu anaondoka, na alikua mtanashati sana hiko kipindi.
Mara akanunua gari, mara akajenga nyumba, yani ni kwa muda mfupi sana amefanya hayo mambo, lakini alikua hataki tuonane. Mimi nilibaki tu na butwaa kwamba kipindi cha shida kule tulikua wote, utamu nampa vizuri alafu amepata mafanikio ananiona mimi takataka, nikawa tu mpole sikua na chakufanya nikamuachia Mungu.
Kuna siku cha ajabu, akanitafuta na kuniomba sana msamaha na kusema kua amebadilika na hatorudia tena kunipotezea, basi na mimi kwakua nampenda, nikampa tena nafasi moyoni mwangu nikijiambia kua amebadilika na maisha yataenda vizuri. Akanipeleka zanzibar, nilifurahi sana kiukweli, ila nilishangaa maana alikua mbahili hatoi pesa lakini alianza kua mwema mpaka nikashangaa, ndo nikajisemea ndo kubadilika kwenyewe huku.
Tulikaa zanzibar kama siku tatu hivi na ijumaa tukarudi dar. jumapili yake kuna rafiki yangu aliniomba tutoke out, ni mmoja wa marafiki zangu watatu ambao nawafahamu dar yaani BFF. basi huyo rafiki ananipeleka sehemu moja hivi nzuri sana, tukala na kunywa, ila kwenye maongezi akaniambia kua kuna kitu anataka kuniambia, nikamwambia sawa nakusikiliza. Akanionesha simu yake ya mkononi nikakuta picha ya mpenzi wangu na yeye wamekumbatiana kimahaba.
Aisee iliniuma ile siku yani $##$๐คฌ alinikera vibaya mno. Lakini nikainuka na kuondoka zangu na urafiki ukaishia hapo hapo na yule mwanaume nikaachana nae maana sasa nilihofia ataniletea magonjwa bure na mauza uza ya kutembea na marafiki zangu. ila kiukweli niliumia sana. Basi siku zikaendelea na maisha yakaendelea.
Katika shughuli zangu nikakutana na mkaka mwingine, alinivutia tukapendana, maana alikua akiniungisha sana biashara zangu na tukazoeana tukawa wapenzi. Penzi likakolea nakwambia, tena alikua akinisaidia kusuport biashara zangu, na hata siku ikiwa mbaya anaelewa na kunisaidia, basi nikasema hapa mume nimepata.
Kila nikimmc nikimpigia simu anapokea, yani alikua kwenye mawasiliano yuko vizuri, lakini aliniambia kua nikitaka kwenda kwake sharti nimwambie kwanza na nisiende bila ruhusa, japo alinipa ufunguo wa nyumba anayokaa. Sasa ikafika tarehe ya birthday yake kwenye mwezi wa kumi hivi, nikataka nimfanyie kitu japo nimnunulie zawadi na keki na nimfanyie surprise.
Zawadi zikafungwa vizuri, mimi nilikua naishi goba, yeye anaishi mikocheni, basi nikavaa vizuri kistaarabu na kwa kupendeza, nikabolt zangu bajaji nikaelekea nyumbani kwake. Nikafika mpaka pale nikaona geti lipo wazi, maana yake yupo na nitamkuta ndani, nikaingia mpaka ndani, nikakuta TV ipo wazi, nikaenda jikoni napo hakukua na mtu.
Nikawa najiuliza kulikoni, atakua wapi, wakati najiuliza, nikawa nasikia sauti ya miguno hivi na ni sauti ya mpenzi wangu ikitokea chumbani na mlango wa chumbani ulikua wazi haujafungwa. Yani moyo ulikua unadunda kwa hofu, hasira yaani sijui nielezeje, nikawaza yani huyu ananicheat mimi, nilijua ni mwanaume mzuri kumbe ni wale wale, tena siku yake ya kuzaliwa leo..
Nikasogea hadi mlango wa chumbani, heee makubwaa, yaniii huwezi amini, yaani mpenzi wangu anafanya mapenzi na mwanaume mwenzake, tena yeye ndo analiwa na huyo jamaa, tena ni libaba kubwaa lina midevu mingii, daaah moyo ulifanya paaaa sikuamini nachokiona. Nilirudi sebuleni na kutoka zangu nje uzuri hawakuniona lakini ndo ikawa mwanzo na mwisho wa mahusiano na yule kaka, alinitafuta sana lakini nilimblock kila sehemu, yani mwanaume shoga unaliwa tena nyumbani kwako kwenye kitanda ambacho nikija ndo unanikula hapo, kumbe na yeye analiwa khaaaaa. iliniuma sana, lakini kwa sasa nimetulia zangu kwanza na haya mambo ya mahusiano.
Keep reading
Sign in to read the full confession
Create an account or log in to unlock the rest of this story.